Sat, 29 Jan 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Goli la Nahodha Aggrey Morris dakika ya 30 limeipa Azam FC ushindi wa 1-0 dhidi ya Transit Camp katika mchezo wa Hatua ya 32 Bora Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) usiku wa jana Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
Kwa ushindi huo, Azam FC inakwenda Hatua ya 16 Bora ya michuano hiyo maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC), ambako itamenyana na timu ya Daraja la Kwanza, Bagamoyo Friends iliyoitoa Catamine.
Tazama hapa Video kuona namna goli hilo lilivyofungwa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live