Wauguzi katika Hospitali ya Wazazi Mwembeladu Zanzibar wamesimamishwa kazi kwa muda wa wiki mbili ili kupisha uchunguzi kufuatia mama kujifungulia mtoto chooni baada ya kupata uchungu akiwa hospitalini hapo kwaajili ya kujifungua.
Wauguzi katika Hospitali ya Wazazi Mwembeladu Zanzibar wamesimamishwa kazi kwa muda wa wiki mbili ili kupisha uchunguzi kufuatia mama kujifungulia mtoto chooni baada ya kupata uchungu akiwa hospitalini hapo kwaajili ya kujifungua. Hata hivyo inadaiwa kuwa akiwa hospitalini hapo wauguzi wa zamu walimtolea maneno ambayo hayakuwa rafiki wala faraja wakati akiugua uchungu na hata alipojifungua walimtaka mama huyo asafishe pale alipojifungulia mtoto wake.