Miili ya Watoto 6 wanafunzi wa Shule ya Msingi Ochuna, waliofariki dunia kwa kuzama na kunasa kwenye tope katika Bwawa la Skimu ya umwagiliaji wa Kijiji cha Ochuna, Wilaya ya Rorya mkoani Mara, inaagwa na kuzikwa jana katika eneo la viwanja vya Shule ya Msingi Ochuna.
Rais Samia Suluhu Hassan ametoa mkono wa pole na rambirambi ya Tsh milioni 30 kufuatia vifo vya Watoto hao ambao wote ni Wasichana.
Akiwasilisha rambirambi hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Rorya Juma Chikoka amesema kwa mujibu wa Rais Samia, fedha hizo zimetolewa kwa kila Familia ya Mtoto aliyefariki dunia, ambapo kila Familia itapata Tsh. milioni tano.
Jana miili hiyo iliagwa na Watoto wanne watazikwa eneo moja.