Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wananchi waandamana jijini Nairobi leo

Video Archive
Tue, 7 Jul 2020 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Polisi jijini Nairobi mchana huu wa Julai 7, 2020, wamelazimika kutumia mabomu ya machozi ili kuwatawanya waandamanaji katika mitaa mbalimbali ya jiji la Nairobi.

Mwandishi wa East Africa Television jijini Nairobi Dennis Chisaka ameripoti kuwa wakazi hao wa Nairobi wameamua kuingia barabarani wakipinga mauaji holela ya raia.

Chisaka amefafanua kuwa waandamanaji wanadai mauaji hayo yanafanywa na polisi.

Hata hivyo hali inazidi kuwa shwari baada ya polisi kudhibiti.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live