Dodoma. Watoto ni baraka. Lakini unapopata watoto zaidi ya wawili ‘pacha’ changamoto huanza kuonekana katika malezi na namna ya kuwatunza kama ilivyotokea kwa Radhia Solomon (24).
Leo Jumatatu Juni 3, 2019 Radhia ametembelea bungeni jijini Dodoma na Spika Job Ndugai akatoa hoja kwa wabunge akitaka waridhie kukatwa posho zao za leo kwa ajili ya kumsaidia Radhia, hoja mbayo imekubaliwa na wawakilishi hao wa wananchi.
Licha ya hoja hiyo kuibua mvutano huku wabunge wakizungumza bila utaratibu, mwisho walikubaliana kuchangia Sh50,000 kwa wabunge wanawake na Sh100,000 kwa wanaume.
Aprili, 2019 Radhia alipewa talaka na muweke ikiwa ni siku 90 tangu ajifungue watoto hao. Alijifungua pacha hao wanne Januari 8, 2019 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).
Spika Ndugai wakati anamtambulisha mwanamke huyo alianza kueleza jinsi anavyopitia katika wakati mgumu, hasa baada ya mumewe kumkimbia.
Soma zaidi: VIDEO: Mama aliyejifungia watoto wanne anena
Pia Soma
- Pongezi ya Nape kwa Waziri Makamba yaibua mjadala
- Watu 14 wauawa kwa bomu Syria
- Jeshi latawanya waandamaji Sudan, wawili wauawa
Pendekezo la mbunge wa Viti Maaum (Chadema), Susan Lyimo kutaka wabunge wanawake kukatwa kiasi hicho na wanaume Sh100,000 ilipitishwa na Ndugai licha ya baadhi ya wabunge kusikika wakipinga akiwemo mbunge wa Nkasi Kaskazini (CCM), Ally Keissy.
Watoto wa Radhia wa kike ni wawili Faudhia na Fardhia na wa kiume wawili Suleiman na Aiman ni pacha ambao kila mmoja alikuwa na mfuko wake wa uzazi.
Soma zaidi: