Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

VIDEO: Profesa Kusiluka ataja sifa za kupata ajira

Video Archive
Fri, 20 Sep 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Profesa Lughano Kusiluka amesema soko la ajira linahitaji watu wanaojiamini, wanaoweza kujieleza na waadilifu.

Profesa Kusiluka ameyasema hayo leo Alhamisi Septemba 19, 2019 katika Jukwaa la Fikra la kampuni ya Mwananchi Communications Ltd (MCL) kujadili kuwezesha vijana kuwa na ujuzi na maarifa mahsusi linalorushwa moja kwa moja na MCL Digital na televisheni ya ITV.

Amesema mitalaa ya taasisi za elimu ya juu nchini inakidhi mahitaji ya soko la ajira lakini changamoto imekuwa ni idadi kubwa ya wahitimu wakati soko la ajira bado ni dogo.

"Lazima tujiulize swali, kwa umoja wetu ni kwa namna gani tutaongeza idadi ya ajira? Ni kwa namna gani tutawaandaa vijana wetu wakiwa bado vyuoni kujiandaa na soko la ajira aidha kwa kujiajiri au kuajiriwa," amesema.

Profesa Kusiluka amesema chuo cha Mzumbe kuna kambi ya mjasiriamali ambayo inatoa fursa kwa wanafunzi kutoa mawazo yao ya ujasiriamali ambayo wanakwenda kufanya baada ya kuhitimu masomo yao.

Kwa upande wake, Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Aga Khan, Veronica Sarungi amesema ni muhimu kumjengea mwanafunzi ari ya ushirikiano na wenzake, hiyo inaongeza ushindani hasa kwenye ujasiriamali.

Habari zinazohusiana na hii

Advertisement
Amewataka vijana kutambua kwamba wana uwezo wa kuibadilisha dunia kwa sababu wengi waliofanya mambo makubwa duniani, walifanya hivyo wakiwa bado vyuoni, tena hawakumaliza hata masomo yao.

"Vijana wajue kwamba ndani yao wana uwezo mkubwa wa kubadilisha maisha yao na vizazi vijavyo. Wasiipuuze nguvu hiyo, waifanyie kazi," amesema Sarungi wakati akichangia mada kwenye Jukwaa hilo.

Chanzo: mwananchi.co.tz