Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini DCP David Misime amewatahadharisha wananchi kutojihusisha na maandamano yanayopangwa kufanywa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) akisema maandamano hayo ni haramu.
Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini DCP David Misime amewatahadharisha wananchi kutojihusisha na maandamano yanayopangwa kufanywa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) akisema maandamano hayo ni haramu. Taarifa hii ya Polisi imetolewa leo septemba 13, ikiwa ni baada ya kauli ya Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) , Freeeman Mbowe kuwataka viongozi wote wa chama hicho nchini kujipanga kuja Dar es Salaam kwa ajili ya kushiriki maandamano mnamo Septemba 23, mwaka huu ikiwa ni sehemu ya kupinga matukio ya utekaji na mauaji yanayoendelea hususiani kwa wafuasi wa chama hicho.