Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

TV

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Singida Black Stars yaendelea kugawa dozi Ligi Kuu

Singidablackstarssc 1729876453886.jpeg Singida Black Stars yaendelea kugawa dozi Ligi Kuu

Fri, 25 Oct 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Timu ya Singida Black Stars imeibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Fountain Gate katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa CCM Liti mjini Singida.

Mabao ya Singida Black Stars leo yamefungwa na viungo Muivory Coast, Josaphat Arthur Bada dakika ya 54 na mzawa, Ayoub Reuben Lyanga dakika ya 65.

Kwa ushindi huo, Singida Black Stars iliyo chini ya Mbelgiji, Patrick Aussems inafikisha pointi 22 katika mchezo wa nane na kuendelea kuongoza Ligi Kuu kwa pointi tatu zaidi ya vigogo, Simba SC baada ya wote kucheza mechi nane.

Kwa upande wao Fountain Gate baada ya kipondo cha leo wanabaki na pointi zao 16 za mechi tisa sasa nafasi ya nne.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: