Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Simbachawene aagiza mkandarasi kuwekwa ndani

102592 Pic+mkanda.png Simbachawene aagiza mkandarasi kuwekwa ndani

Wed, 15 Apr 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dodoma. Waziri wa Mambo ya Ndani nchini Tanzania,  George Simbachawene ameagiza Mohamed Nangonga ambaye ni mhandisi wa kampuni ya Nangonga Ltd kukamatwa kwa madai ya uzembe  wa kutoweka alama za barabarani na kusababisha vifo vya watu watatu.

Mkandarasi  huyo anasimamia kuweka viraka katika eneo la Ihumwa jijini Dodoma barabara ya Dodoma- Morogoro.

Akizungumza leo Jumatano Aprili 15, 2020, Simbachawene amesema kampuni hiyo imechimba mashimo katika eneo hilo na kuyaacha muda mrefu bila kuweka alama.

Amesema uwepo kwa mashimo hayo umesababisha ajali mbili na watu watatu kupoteza maisha.

"Wewe ni rafiki yangu lakini katika hili ni lazima uwajibike, unachimba mashimo barabarani huweki alama ili wenye magari wajue kuna matengenezo yanayofanyika.”

"Nilipita juzi hapa nikaona haya mashimo nikasema yanaweza kukaa muda mrefu bila kutengenezwa  matokeo yake sasa kunatokea vifo huu ni uzembe, naagiza mkandarasi huyu akamatwe pamoja na vibarua wake,” amesema Simbachawene.

Pia Soma

Advertisement

Baada ya agizo la waziri mkandarasi huyo aliwekwa chini ya ulinzi na askari polisi waliokuwepo eneo la tukio.

Chanzo: mwananchi.co.tz