Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Serikali yatangaza ajira za walimu 13,000 (+video)

Video Archive
Sat, 28 Nov 2020 Chanzo: millardayo.com

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhandisi Joseph Nyamhanga ,ametangaza ajira za walimu wa shule za msingi na Sekondari zipatazo 13,000 huku akiwataka wote walioweza kupata ajira hizo kuripoti ndani ya muda uliopangwa.

Akitangaza mbele ya waandishi wa habari jijini Dodoma Mhandisi Nyamhanga amesema kuwa walimu hao wanapaswa kuripoti ndani ya siku 14 kuanzia Desemba Mosi hadi 14 na wale ambao watashindwa kuripoti ndani ya muda huo nafasi zao zitachukuliwa na walimu wengine.

Mhandisi Nyamhanga amewataka wote walioteuliwa kuripoti kwenye vituo vyao vya kazi ambavyo ni shule za msingi na sekondari na siyo kuripoti katika ofisi za halmashauri huku akitoa onyo kwa wale watakaochukua posho za kujikimu kwa siku saba watakazoenda kuripoti afu wasitokee kuwa watachukuliwa hatua za kisheria.

Amesema kuwa maombi yote yalitumwa kwa njia ya mtandao na mchakato wa kuyapata majina ya waliokidhi vigezo ulihusisha wataalamu kutoka TAMISEMI na idara mbalimbali.

Chanzo: millardayo.com