Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rais Samia kuhutubia Bunge April 22 (+video)

Video Archive
Tue, 20 Apr 2021 Chanzo: millardayo.com

Rais Samia Suluhu Hassan atahutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Aprili 22, 2021.

Spika wa Bunge, Job Ndugai amelitangazia Bunge leo Jumatatu Aprili 19, 2021 kuwa Rais Samia atalihutubia Bunge Alhamisi ya wiki hii kuanzia saa 10 jioni.

Hivyo, Spika Ndugai amewaagiza wabunge wote walioko nje ya Jiji la Dodoma kurudi na wale wanaotaka kuondoka wazingatie kuwapo kwa shughuli hiyo kwanza.

Rais Samia atalihutubia Bunge kwa mara ya kwanza tangu alipoapishwa kuwa Rais Machi 19, 2021 baada ya kifo cha Rais wa tano, John Magufuli kilichotokea Machi 17, 2021.

Chanzo: millardayo.com