Menu ›
Habari
Sat, 15 Oct 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amezuru na kuomba dua kwenye Kaburi la Rais wa Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli nyumbani kwake Chato Mkoani Geita.
Samia amezuru kaburi hilo leo, Jumamosi tarehe 15 Oktoba, 2022 wakati akiwa ziarani mkoani humo baada ya kumaliza ziara yake ya siku mbili mkoani Kagera.
Magufuli alifariki dunia Machi 17, 2022 wakati akipatiwa matibabu jijini Dar es Salaam na Machi 19, mwaka huo huo, Samia aliapishwa kushika wadhifa huo kutokana na katiba ya Tanzania.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live