Rais Samia, Mapema Oktoba 15, 2021 ameweka jiwe la msingi katika Hopsitali ya Mawenzi Mkoani Kilimanjaro wakati akizindua jengo la Mama na Mtoto ambalo limefikia asilimia 70 kukamilika.
Ujenzi wa jengo hilo umegharimu jumla ya shilingi bilioni 6 ambazo zimetolewa kwa awamu mbili na tayari fedha za awamu ya kwanza zimeshatolewa.
"Najua kulikuwa na mkwamo kidogo, ila tayari tumeshaweka bilioni 3, na zilizobaki tutazimalizia, jengo hili halikuwa na hadhi inayofaa kwa maana ya hospitali" Rais Samia
Mbali na hayo, Rais Samia amewataka watumishi hao wa umma kufanya kazi kwa bidii kwani Serikali imeshaanza kushughulikia maslahi yao pamoja na kuwapandisha vyeo.