Rais Samia Suluhu Hassan ameridhia stesheni ya Reli ya Kisasa ya SGR ya mkoani Dodoma kuitwa jina lake na sasa itajulikana kama Samia Station huku stesheni ya Dar es Salaam ikipewa jina la mtangulizi wake, Hayati Dkt. John Pombe Magufuli.
Rais Samia Suluhu Hassan ameridhia stesheni ya Reli ya Kisasa ya SGR ya mkoani Dodoma kuitwa jina lake na sasa itajulikana kama Samia Station huku stesheni ya Dar es Salaam ikipewa jina la mtangulizi wake, Hayati Dkt. John Pombe Magufuli. “Kituo cha Dar es salaam pale kwenye jumba la Tanzanite pale tutalipa jina la Magufuli kwa sababu ndiye ameanza ujenzi,” amesema Rais Samia Suluhu akizindua rasmi treni ya SGR Dar es Salaam - Dodoma.