Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Nurdin Babu amethibitisha kutokea kwa vifo vya Watu 14 vilivyotokea katika eneo la Kikavu Wilayani Hai Mkoani Kilimanjaro baada ya gari la kubeba aina ya Toyota Coaster kugongana uso kwa uso na Lori la mizigo.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Nurdin Babu amethibitisha kutokea kwa vifo vya Watu 14 vilivyotokea katika eneo la Kikavu Wilayani Hai Mkoani Kilimanjaro baada ya gari la kubeba aina ya Toyota Coaster kugongana uso kwa uso na Lori la mizigo. Chanzo cha ajali hiyo bado hakijajulikana hadi sasa lakini idadi ya vifo ni 14 ambapo Watu sita walifariki dunia papohapo kwenye eneo la ajali na wengine nane wamefariki wakati wakiwaishwa Hospitali.