Menu ›
Habari
Mon, 4 Jun 2018
Chanzo: bongo5.com
/>
Mapacha hao ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakisumbuliwa na matatizo ya moyo walilazwa tangu mwezi Disemba mwaka jana katika hospitali ya mkoa ya Iringa.
Hata hivyo, baadae walihamishiwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKIC) katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, ambapo walikaa kwa miezi miwili kwa ajili ya matibabu mpaka waliporuhusiwa kurejea tena Iringa mnamo Mei 17, 2018 .
Mapacha hao walizaliwa wilayani Makete mkoani Njombe mwaka 1996 na walihitimu darasa la saba katika shule ya msingi Ikonda, kisha wakajiunga na shule ya Maria Consolata iliyopo Kilolo mkoani Iringa ambapo walihitimu kidato cha nne.
Maria na Consolata, walijiunga na shule ya Sekondari ya Udzungwa wilani Kilolo na kuhitimu kidato cha sita, ambapo walifanikiwa kusonga mbele na kujiunga na Chuo Kikuu cha Katoliki cha Ruaha (Rucu) walipokuwa wakisomea fani ya ualimu.
Kufuatia vifo hivyo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ametoa salamu za rambi rambi kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki wa mapacha hao.
Mhe Rais @MagufuliJP ametoa pole kwa familia ya mabinti hawa ambao wamefariki dunia jana.Mola aziweke roho zao mahali pema peponi. Amen. pic.twitter.com/5x9ZRhm2sI
— Msemaji Mkuu wa Serikali (@TZMsemajiMkuu) June 3, 2018
Loading...
Chanzo: bongo5.com