Menu ›
Habari
Wed, 31 Jul 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Shirika la Reli Tanzania (TRC) limeripoti hitilafu ya umeme kwenye treni yake ya kisasa ya SGR iliyosababishwa na wanyama aina ya ngedere na bundi.
Kulingana na TRC, hitilafu hiyo iliilazimu treni ya SGR kusitisha safari zake kati ya Dar es Salaam na Dodoma kwa saa mbili.
"Taarifa za awali zinaonesha kuwa hitilafu za aina hiyo husababishwa na wanyama (ngedere) au ndege (bundi) wanapogusa nyaya za umeme zilizotandazwa juu ya reli (overhead catenary system)," TRC.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live