Menu ›
Habari
Mon, 22 Jul 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rais Samia Suluhu Hassan, amemteua Deogratius Ndejembi kuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
Awali, alikuwa Waziri Ofisi Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) ambapo ameteuliwa Ridhiwani Kikwete kuwa waziri.
Ndejembi ambaye ni Mbunge wa Chamwino (CCM), Dodoma amechukua nafasi ya Jerry Silaa aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari.
Silaa ambaye ni Mbunge wa Ukonga, amechukua nafasi ya Nape Nnauye ambaye uteuzi wake umetenguliwa.
Uteuzi huo umefanyika jana Jumapili, Julai 21, 2024.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live