Menu ›
Habari
Mon, 22 Jul 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ametengua uteuzi wa mawaziri wawili, Nape Nnauye (Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari) na January Makamba wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Mbali na hao, Rais Samia ametengua uteuzi wa Stephen Byabato aliyekuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Utenguzi huo umefanyika usiku huu wa leo Jumapili, Julai 21,2024 kupitia taarifa kwa umma iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live