Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mbunge Akiri Kutumia Bangi: Ina faida Nyingi - Video

Video Archive
Thu, 3 Jun 2021 Chanzo: globalpublishers.co.tz

Mbunge Akiri Kutumia Bangi: Ina faida Nyingi – Video June 3, 2021 by Global Publishers



MBUNGE Iringa Mjini, Jesca Msambatavangu amekiri kuwa akiwa na umri mdogo aliwahi kutumia majani na Mbegu za Bangi kama mchanganyiko wa Chakula Bora.

“Uwezo wa kufikiri wa wazee wa zamani ni tofauti na vijana wa sasa. Ninaweza kuonekana mnene, ni bonge lakini nina udumavu unakuja kuleta athari sana kwenye uwezo wa kufirki na kutoa maamuzi.

“Kijana hajui kama anataka kuoa au lah, binti hajui kama anataka kuolewa au hataki, unamuona ni binti lakini anafanya mambo ya kimama.

“Wakati nikiwa kwa bibi mkoani Iringi, sisi bangi tulikuwa tukitumia majani yake kama mbona, Kamba zake tulikua tukitumia kutengeneza mikeka, mbegu zake zilikuwa zikitumika kama kiungo cha mboga akipewa mama aliyejifungua maziwa yanatoka kama yote.

“Kwa hiyo kabla ya kuzuia tungefanya tafiti kwanza, tusitazame tu madhara tuangalie na faida zake kwa jamii yetu,” amesema Jesca.

Chanzo: globalpublishers.co.tz