Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mbowe "TRA wameondoa zuio la akaunti zangu" (+video)

Video Archive
Mon, 12 Apr 2021 Chanzo: millardayo.com

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Freeman Mbowe ametaja sababu ya kuamua kuondoka nchini na kwenda kuwekeza nchi zingine kuwa ni tozo ya kodi kiasi cha Sh2 bilioni aliyopewa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

“Mwaka 2018 nikiwa Gerezani Segerea, TRA waliandika barua kwangu kwamba Kampuni yangu moja inadaiwa kodi ya Bilioni mbili kitu ambacho sio Kweli wakafunga akaunti zangu, Juzi pengine baada ya kauli za Mama Samia, TRA wameniandikia kuwa tumeondoa zuio la akaunti zako, tunafungua”———Mwenyekiti wa CHADEMA- Taifa, Freeman Mbowe akihutubia leo Dar es salaam

“Sababu mojawapo iliyonifanya niende Nchi za nje nilienda kutafuta uwekezaji, ni kama sikuruhusiwa kufanya biashara Tanzania, kila biashara niliyojaribu kuifanya ilizuiwa, ilibomolewa, nikaona naweza kufanya biashara Dubai, South Afrika n.k, sasa Mimi ni Mbowe, je wangapi wamekimbia kuwekeza Tanzania?”———MBOWE

Chanzo: millardayo.com