Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Makonda: Tumetoka Ngorongoro na ushindi

Makonda Ngorongoro Mz Makonda: Tumetoka Ngorongoro na ushindi

Wed, 28 Aug 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Christian Makonda amemtaja Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kama kiongozi mwenye hekima na busara ya kiwango cha juu katika kudumisha amani,umoja na mshikamano wa Watanzania.

Makonda ametoa kauli hiyo leo Agosti 28, 2024 alipokuwa akiwakaribisha wakuu wa Taasisi na mashirika ya Umma, wanaokutana Jijini Arusha kwenye kikao kazi cha kuelekezana na kushirikishana mabadiliko ya kiutendaji kwenye taasisi na mashirika ya Umma nchini.

Ametoa kauli hiyo kauli mara baada ya serikali ya Rais Samia kufanikiwa kuumaliza mgogoro uliokuwepo kwa wakazi wa wilaya ya Ngorongoro, baada ya kutoa maelekezo kupitia kwa mawaziri walioambatana na Mhe. Makonda wiki iliyopita kwenda kuzungumza na wananchi wa Ngorongoro na kuondoa vikwazo na visababishi vya sintofahamu iliyokuwepo.

“Hekima hizo mheshimiwa Rais ni za aina yake na busara zako ni za kipekee kwani zimetufanya tuondoke Ngorongoro kama washindi. Wilaya ya Ngorongoro sasa kuna amani, Arusha ina amani, Asante Rais Samia,” amesema Paul Makonda.

Katika hatua nyingine, Makonda amewaalika viongozi hao kuwekeza mkoani Arusha kutokana na mahitaji makubwa ya kumbi za mikutano, hoteli na hospitali za kisasa zitakazosisimua utalii wa matibabu kwenye mkoa huo kinara kwa utalii kwa upande wa Tanzania bara.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live