Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Majaliwa ataka ofisi ya Mwanasheria Mkuu iwe kila mkoa

40452 Waziripic Majaliwa ataka ofisi ya Mwanasheria Mkuu iwe kila mkoa

Thu, 7 Feb 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dodoma. Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa ameitaka ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuhakikisha inakuwa na ofisi zake katika  kila mkoa nchini.

Majaliwa  alitoa wito huo juzi alipotembelea banda la ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika maonyesho ya wiki ya sheria yanayoendelea katika  viwanja vya  Mwalimu Nyerere 'Square' Jijini Dodoma.

"Kwa kuwa sasa mna muundo mpya na majukumu yenu yameongezeka yakiwamo ya uratibu na utoaji wa ushauri wa kisheria, itakuwa vema kuwa na ofisi kila mkoa ili wananchi wasisafiri umbali mrefu kwenda kutafuta au kuomba ushauri wa jambo la kisheria," alisema.

Waziri Mkuu alisema anaamini baada ya ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuundwa upya inakuwa na nafasi nzuri ya kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi na kwa tija.

Akitoa maelezo kwa Waziri Mkuu, kuhusu majukumu ya ofisi ya Mwanasheria Mkuu, Kaimu Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Said Nzori alisema baada ya mabadiliko ya ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, ofisi hiyo imekuwa na divisheni za kisheria tatu.

 



Chanzo: mwananchi.co.tz