Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema kuwa ni jukumu la kila Mtanzania kuzingatia mahubiri ya viongozi wa dini ili nchi iendelee kuwa na amani ili maendeleo yaendelee kuonekana.
Aliyasema hayo leo alipohudhuria sala ya Ijumaa katika msikiti wa Buhari uliopo Ruangwa, mkoani Lindi. Waziri Mkuu amesema ni muhimu Watanzania wakajenga tabia ya kuaminiana, kuvumiliana pamoja na kupendana kwani mambo haya yote huchangia uwepo wa amani na utulivu.
"Nchi yetu imekuwa na kasi ya maendeleo katika maeneo mengi. Mimi naamini maendeleo haya yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na amani tuliyonayo na hii inatokana na mahubiri ya viongozi wetu wa dini. Dini ina mchango mkubwa sana katika uendeshaji wa Serikali," amesema