Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli leo Juni 19, 2020 ametengua uteuzi wa viongozi watatu wa Mkoa wa Arusha na kufanya uteuzi wa viongozi watakaoshika nyadhifa zao.
Taarifa hiyo imetolewa kwa vyombo vya habari kutoka kurugenzi ya mawasiliano ya Rais Ikulu amabayo inaeleza kuwa, Kwanza Mhe. Rais Magufuli ametengua uteuzi wa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo na amemteua Idd Kimanta kuwa mkuu wa mkoa huo.
Kabla ya uteuzi huo Idd Kimanta alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Monduli Mkoani Arusha na nafasi ya Mkuu wa Wilaya ya Monduli itajazwa baadaye.
Kwa kutengua uteuzi wa pili na watatu unaweza kusoma kwenye barua hapo chini.