Dar es Salaam. Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli amemteua Dk Leonard Chamriho kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Uwekezaji wa Mapato ya Mafuta na Gesi (Portfolio Investment Advisory Board).
Dk Chamriho ni Katibu Mkuu wa Uchukuzi katika Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.
Pamoja na uteuzi wa Mwenyekiti, Rais Magufuli amewateua wajumbe wanne wa bodi hiyo ambao ni;
- Casmir Sumba Kyuki (Katibu Mtendaji wa Tume ya Kurekebisha Sheria).
- Dk Suleiman Magesa Missango (Mkurugenzi wa Utafiti wa Uchumi na Sera wa Benki Kuu ya Tanzania – BOT).
- Safiel Fahamuel Msomvu (Kaimu Meneja Uwekezaji wa Shirika la Maendeleo ya Petrol Tanzania – TPDC).
- Dk Mussa Daniel Budeba (Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam – UDSM).
Taarifa iliyotolewa leo Alhamisi Septemba 26, 2019 na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu ya Tanzania imemnukuu Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi akisema uteuzi wa Dk Chamriho na wajumbe hao ulianza Septemba 25, 2019.
Pia Soma
- Sababu mawaziri kuandamana pamoja kuzungumza na wafanyabiashara hizi hapa
- Askari wawili JWTZ wafariki ajalini, 20 wajeruhiwa
- VIDEO: Wanafunzi 13 wazuiwa kuendelea darasa la saba kwa kutofanya mtihani darasa la nne
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
26 Septemba, 2019