Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mabula azichongea halmashauri kwa Majaliwa

95701 Mabula+pic Mabula azichongea halmashauri kwa Majaliwa

Fri, 14 Feb 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dodoma. Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi nchini Tanzania, Angelina Mabula amesema Serikali ilitoa mkopo usio na riba kwa halmashauri 24 nchini lakini ni halmashauri nne tu ndizo zilizotekeleza.

Mabula ameyasema hayo leo Alhamisi  Februari 13,  2020 katika uzinduzi wa Mpango Kabambe wa Jiji la Dodoma uliozinduliwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

Amesema halmashauri hizo zilipewa mkopo wa Sh6.2 bilioni,

“Sababu kubwa ya kutotekeleza kwa halmashauri hizo ni kutokuwa waaminifu.”

Amezitaja halmashauri hizo kuwa ni Mbeya, Kahama, Ilemela na Bariadi.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma,  Dk Binilith Mahenge amemuomba Majaliwa kutoa motisha kwa wawekezaji katika jiji la Dodoma.

Pia Soma

Advertisement
Amesema kutokana na Serikali kuhamia Dodoma mahitaji ya huduma mbalimbali za kijamii kama hoteli za nyota tano, shule za kimataifa zitahitajika.

Hoja hiyo iliyoungwa mkono na Mbunge wa Dodoma Mjini (CCM), Anthony Mavunde aliyesema kuendelea kwa jiji la Dodoma kunahitaji ushirikiano kati ya Sekta binafsi na Serikali.

Ameiomba Serikali kutumia Sheria ya mwaka 1989 ambayo ilitoa unafuu kwa wawekezaji.

Amesema kitendo cha mpango huo kutogusa kuhamisha wakazi 4,000 wa kata ya Mtumba jijini hapa kumewafanya wakazi wa eneo hilo waliokuwa na hofu kumalizika.

Chanzo: mwananchi.co.tz