Rais Samia, anazungumza na wananchi katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Ushirika Wilayani Moshi akiwa kwenye ziara yake ya kikazi ya siku mbili mkoani Kilimanjaro.
Rais Samia, anazungumza na wananchi katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Ushirika Wilayani Moshi akiwa kwenye ziara yake ya kikazi ya siku mbili mkoani Kilimanjaro. Kabla ya kufika katika viwanja hivyo, Rais Samia alizindua miradi ya maendeleo ambayo ni uzinduzi wa barabara ya Sanyajuu yenye Km 32.2 pamoja na kuweka jiwe la msingi katika hospitali ya Mawenzi kwenye jengo la mama na mtoto na kuweka jiwe la msingi kwenye daraja la Rau ambalo lilivunjika siku za nyuma.