Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kilio cha bando kuisha kabla ya muda, Waziri atoa maagizo (+video)

Video Archive
Thu, 24 Dec 2020 Chanzo: millardayo.com

Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dk Faustine Ndugulile amelielekeza Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Mawasiliano (TCRA- CCC) kufanya tathmini ya malalamiko yanayotolewa na wananchi dhidi ya kampuni za simu kuhusu kukatwa na kuibiwa vifurushi ili kupata ufumbuzi wa tatizo hilo.

“Wananchi wanamalalamika kuhusiana na mabando yao kuisha kwa wakati, wanalalamika kubadilishiwa gharama za matumizi ya mabando yao, wanalalamika kupunjwa mabando yao, wanalalamika kuhusu fedha wanazotuma yote yanahitaji majibu”

“Yote yanahitaji kupatiwa matibabu kwahiyo nimewaelekeza Baraza husika kuhakikisha kwamba hatufanyi kazi kwa mazoea”-Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dr.Faustine Ndugulile

Chanzo: millardayo.com