Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kauli ya Kagame kabla ya wanajeshi wake 4 kuuawa Msumbiji

Video Archive
Wed, 29 Sep 2021 Chanzo: millardayo.com

Wanajeshi wanne wa Rwanda wameuawa na wengine 14 wamejeruhiwa katika Oparesheni ya kijeshi dhidi ya Wanamgambo wenye itikadi kali nchini Msumbiji katika Jimbo la Cabo Delgado, hii imetokea zikiwa zimepita siku chache tangu Rais wa Rwanda Paul Kagame alipokwenda Msumbiji na kukutana na Rais wa Msumbiji Filippo Nyusi ambapo kwa pamoja waliwapongeza Wanajeshi wa Nchi zao kwa kupambana na Kikundi hicho.

Hii ni mara ya kwanza kwa Rwanda kutangaza majeruhi katika kikosi chake cha Wanajeshi 1,000 tangu waanze Oparesheni nchini Msumbiji.

Jumamosi iliyopita Rais wa Msumbiji na Rais wa Rwanda walikuwa wanawapongeza Wanajeshi ambao wamejitoa kupambana na Wanamgambao hao.

Chanzo: millardayo.com