Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kambi ya upasuaji wa moyo kufanyika Jakaya Kikwete

Wataalam Wa Magonjwa Ya Moyo Wa JKCI Wajifunza India Kambi ya upasuaji wa moyo kufanyika Jakaya Kikwete

Wed, 4 Sep 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto kutoka Kituo cha Mfalme Salman cha Misaada ya Kibinadamu nchini Saudi Arabia, Omar Almohzy, ametembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ili kufanya maandalizi ya kambi maalumu ya upasuaji wa moyo kwa watoto.

Katika picha hii, Dr. Almohzy akimfanyia mtoto kipimo cha echocardiography (ECHO) ili kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi, hatua muhimu kabla ya upasuaji.

Kambi hii itaanza rasmi tarehe 05 Septemba 2024 na inatarajiwa kudumu kwa siku saba. Watoto 30 wanatarajiwa kufanyiwa upasuaji wa moyo wakati wa kambi hii, ambayo inalenga kutoa huduma muhimu kwa watoto wenye matatizo ya moyo.

Aidha, kambi hii inatoa fursa ya kipekee kwa watoto kupata huduma za hali ya juu za upasuaji wa moyo bila gharama kubwa, huku ikionyesha ushirikiano mkubwa kati ya mashirika ya kimataifa na kitaifa katika kuboresha afya za watoto. #KonceptTvUpdates

Chanzo: www.tanzaniaweb.live