Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Huyu ndiye mjane wa marehemu Rais John Pombe Magufuli na watoto wao

E3f95aba5252c386 Huyu ndiye mjane wa marehemu Rais John Pombe Magufuli na watoto wao

Wed, 24 Mar 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

John Pombe Magufuli, Rais wa tano wa Jamhuri ya Tanzania, alifariki dunia katika hospitali ya Moyo ya Mzena jijini Dar es Salaam na kifo chake kutangazwa Jumatano, Machi 17.

Rais ameacha mjane Mama Janeth Magufuli na watoto wawili ambao siku zote wamechagua kuishi maisha ya siri mbali na macho makali ya umma.

Mke wa Magufuli, Janeth anajulikana sana nchini Tanzania kwani amekuwa mke wa Rais wa nchi tangu 2015. Yeye ni mwalimu wa zamani alivyokuwa Magufuli na kabla ya kuwa mama wa taifa, alikuwa mwalimu mzuri katika moja ya shule zinazoongoza nchini humo.

Alikuwa mwalimu katika Shule ya Msingi Mbuyuni iliyoko Dar es Salaam, ambapo aliyekuwa mke wa Rais Salma Kikwete pia alikuwa akifundisha. Alifundisha Jiografia, Historia na Habari Mawasiliano na Teknolojia (ICT) na alijulikana kwa kuwa mchapa kazi kama mume wake.

Ndoa yaoJaneth Magufuli, 61, alifunga ndoa na Magufuli katika harusi iliyofanyika katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) miongo kadha iliyopita. Kulingana na ripoti, wakati wa harusi TUKO.co.ke imeng'amua kuwa rais hakuwa na suti wala pete ya kumvalisha mpenzi wake.

Akiongea Novemba 1, 2018 katika mdahalo uliofanyika UDSM kutathmini miaka mitatu ya uongozi wake wa nchi rais alisema: "Siku niliyooa watu wengi hawakujua…na haimaanishi sikuwa na pesa ya kununua koti au gauni la harusi kwa mke wangu, sikuona kama vitu hivyo ni vya msingi sana."

"Tulienda hapo kanisani pete tukanunuliwa na Padre, tena zilikuwa za shaba. Padre pia alitununulia soda, nakumbuka mimi nilikunywa pepsi na mke wangu alikunywa mirinda...Baada ya hapo nikaenda zangu lab (maabara) kuendelea na shughuli zangu."



Katika ndoa yao, walibarikiwa watoto wawili John Magufuli ambaye amepewa jina la baba yake na mwingine ambaye ni kifunga mimba ni Jessica Magufuli, mwanadada ambaye pia hajulikani sana kwa umma wa Tanzania.



TUKO.co.ke inachukua fursa hii kuitakia familia amani wakati huu mgumu wa maombolezo. Lala salama Magufuli.

Mwandishi ni Ali Hassan Kauleni, Kaunti ya Nairobi

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama taarifa kemkem za TUKO hapa

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke