Msanii wa muziki Bongo, Christian Bella ametangaza kuanza kutoa nafasi kwa vijana katika band ya Malaika.
Muimbaji huyo ambaye anatamba na ngoma ‘Shuga Shuga’, ameimbia The Base, ITV kuwa katika kuongeza nguvu kwenye team yake anatoa fursa kwa vijana wenye uwezo wa kuimba live, kupiga gita na kinanda.
“Nahitaji pia kuboresha team, kijana yeyote mwenye talent ya kuimba live kuna fursa ya kazi kwangu, namkaribisha, awe mpiga gita, awe mpiga kinanda anicheki tu kwenye Instagram yangu” amesema.
Bella ameongeza kuwa si kwamba sasa hana wa kufanya nao kazi ila anachotoka ni kuiboresha zaidi Malaika Music Band.