Kamishna na Polisi Utawala na Menejimenti ya Rasilimali Watu (CP) Suzan Kaganda amezungumzia uzoefu wa Tanzania katika kutekeleza mpango wa polisi jamii na namna ambavyo wananchi wanashiriki kuimarisha usalama.
Kamishna na Polisi Utawala na Menejimenti ya Rasilimali Watu (CP) Suzan Kaganda amezungumzia uzoefu wa Tanzania katika kutekeleza mpango wa polisi jamii na namna ambavyo wananchi wanashiriki kuimarisha usalama. Kaganda amesema suala la amani ni jambo ambalo linatakiwa kushirikisha Jamii ili amani na utulivu wa eneo husika kuimarika. Amesema ushiriki kamili wa wananchi katika ulinzi wa amani husaidia vyombo vya ulinzi kutimiza wajibu wao.