Menu ›
Habari
Mon, 22 Jul 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Balozi Mahmoud Thabit Kombo kuwa Mbunge na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Kabla ya uteuzi huo, Balozi Kombo alikuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, anachukua nafasi ya January Makamba ambaye uteuzi wake umetenguliwa.
Uteuzi huo umefanyika usiku huu wa leo Jumapili, Julai 21,2024 kupitia taarifa kwa umma iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live