Baba mzazi wa mapacha na wanachuo wa Chuo cha Mipango Kampasi ya Mwanza waliofariki wakiogelea katika Ziwa Victoria amesimulia mazito kuhusu watoto wake kabla ya umauti kumfika.
Baba mzazi wa mapacha na wanachuo wa Chuo cha Mipango Kampasi ya Mwanza waliofariki wakiogelea katika Ziwa Victoria amesimulia mazito kuhusu watoto wake kabla ya umauti kumfika. Akizungumza wakati wa misa ya kuwaaga pacha hao ambao ni Lenny na Kenny Makomonde (24) iliyofanyika jana jioni Mei 29, 2023 katika ukumbi wa chuo Baba mzazi Makomonde Deusdedith amesema mara ya mwisho aliwakataza mapacha hao kuacha tabia ya kwenda kuogelea ziwani.