Menu ›
Habari
Fri, 12 May 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambaye pia Mbunge wa Jimbo la Mtama Mhe. Nape Nnauye ameeleza namna ambavyo amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Bernard Membe ambaye aliwahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Mtama kuanzia Mwaka 2002 - 2015
Nape ameyasema hayo leo Bungeni wakati akihojiwa na waandishi wa Habari, ambapo amesema kuwa Marehemu Membe atakumbuka kwa mazuri mengi aliyoitendea nchi
Bernard Membe amefariki dunia leo Mei 12, 2023 katika hospitali ya Kairuki Jijini Dar es Salaam.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live