Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

48 wafariki Nigeria baada ya lori la mafuta kuhusika katika ajali - VIDEO

Video Archive
Mon, 9 Sep 2024 Chanzo: Bbc

Takriban watu 48 wamefariki baada ya lori la mafuta kulipuka lilipogongana na gari lingine kaskazini mwa Nigeria.

Kulingana na mamlaka, lori hilo la mafuta liligongana na lori lingine lililokuwa limebeba wasafiri na ng'ombe, 50 kati yao waliteketezwa wakiwa hai

Shirika la Usimamizi wa Dharura la Jimbo la Niger lilisema kuwa magari mengine kadhaa yalihusika katika ajali hiyo.

Abdullahi Baba-Arab, mkurugenzi mkuu wa Usimamizi wa Dharura wa Jimbo la Niger, alionyesha kuwa waathiriwa walikuwa wamezikwa kwa wingi.

Gavana wa jimbo hilo Mohammed Bago aliwataka madereva kuchukua tahadhari na kuzingatia kanuni za barabarani ili kuzuia majanga hayo.

Ajali mbaya za barabarani zinazohusisha magari ya mafuta hutokea mara kwa mara nchini Nigeria, huku ajali 1,531 zikirekodiwa mwaka 2020 pekee, na kusababisha vifo vya watu 535 na wengine 1,142 kujeruhiwa, kulingana na Kikosi cha Kitaifa cha Usalama Barabarani.

Kampuni ya mafuta inayomilikiwa na serikali ya Nigeria, NNPC Ltd, hivi karibuni ilitekeleza ongezeko kubwa la bei ya petroli kwa asilimia 39, na kuashiria ongezeko la pili kubwa katika zaidi ya mwaka mmoja.

Hata hivyo, licha ya marekebisho hayo, uhaba wa mafuta unaendelea kushuhudiwa, foleni ndefu za magari zikionekana katika miji mikubwa na miji kote nchini.

Chanzo: Bbc